Mtandao huu bado upo kwenye matengenezo, punde utapata matukio katika picha, habari, makala na taarifa mbali za kijamii...Endelea kutufuatilia

Monday, May 28, 2018

Ukosefu wa maji na pedi shuleni unavyo mfedhehesha msichana awapo shuleni



Na Grace Mwakalinga, Mbeya
 “Kutokana na ukata wa fedha kutoka kwa wazazi wakati mwingine ninalazimika kutumia vitambaa ili kujisitiri, kwa siku ninatumia vitambaa vitatu mpaka vinne kulingana na hedhi inavyotoka, wakati wa mapumziko au nikiona nimezidiwa naenda chooni kubadilisha kitambaa kingine, sijisafishi ninavaa hivyovyo kwa sababu ya tatizo la maji hapa shuleni.” alisema Nchambi Petro, ambaye ni Dada Mkuu wa Shule ya Sekondari Imezu iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mkoani Mbeya, katika mahojiano na mwandishi wa Makala hii.
Petro ni Dada Mkuu wa Shule,  ambaye naye anaishi hosteli anadai ukosefu wa huduma ya maji  kunaathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya masomo yao kwani  hutumia muda mwingi kutafuta huduma ya maji kwenye mifereji na mito ambaye iko mbali na mazingira ya shule.
Petro anasema njia pekee ya kutatua changamoto hiyo ni  Serikali au wazazi kukubali kuweka matanki ya kuvuna na kuhifadhi maji katika shule yao wakati wa Mvua.
Wanafunzi  wa kike katika Shule ya Sekondari Imezu,  iliyopo katika Kata ya Inyala  Wilaya Mbeya, wengi wao wanatoka katika familia za kawaida  ambazo pia kipato cha wazazi ni kidogo.  Wengi wanashindwa kujisitiri na kufanya usafi wa maumbile yao kutokana na changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama shuleni hapo.
Wanafunzi hao wanadai kukosekana huduma ya maji kunachangia kwa kiasi kikubwa watoto wa kike  wanapokuwa kwenye hedhi kutoa harufu mbaya  kutokana na kukosa maji ya kujisafisha.
wasichana wa shule za Sekondari wakionesha Pedi ambazo wamepatiwa kama msaada kuwawezesha kuhudhuria masomo vizuri.
Wanasema wakati mwingine wakiwa shuleni hulazimika kuficha kiasi kidogo cha  maji ambayo wamechota  mtoni kwa ajili kujisafishia ili kukwepa fedheha mbele za wanafunzi wa kiume.
Tangu kuanza kwa kidato cha kwanza mwaka 2007, Shule hiyo haijawahi kupata huduma ya maji safi na salama licha ya kuwa na miundombinu ya mabomba ambayo hayatoi maji, hali inayowalazimu wanafunzi kuvunja vipindi vya masomo kufuata huduma ya maji kwenye mito na mifereji.
Licha ya  Shule ya Sekondari Imezu kujenga  mabweni kwa ajili ya watoto wa kike kwa lengo la  kuondoa changamoto za mimba kwa wanafunzi wanaotoka mbali, visa vya ubakaji na kuongeza ufaulu, lakini muitikio wa wazazi au walezi kupeleka hosteli watoto wao umekuwa mdogo kutokana na  changamoto ya maji.
Madhira ya maji shuleni hapo pia yametajwa na wanafunzi kuongeza utoro kwani wakati mwingine hulazimika kuondoka shuleni kutafuta maji ya kunywa matokeo yake  wanafunzi  kutorudi tena kwenye vipindi vingine vya masomo.
Sharon Msalilwa ni mwanafunzi wa kidato cha Tatu katika Shule hiyo ambaye anaishi hosteli anasema  changamoto ya maji imekuwa moja ya kikwazo kwa mtoto wa kike katika kupata elimu kwani awapo kwenye hedhi hukosa amani na morali ya kusoma.
Anasema wakati wa kipindi cha hedhi anashindwa kuzingatia masomo kwani muda wote anajihisi kuwa amechafuka au kuhadhirika mbele ya darasa licha ya kuwa amejisitiri.
Msalilwa anaongeza kuwa kukosekana kwa chumba maalum cha kubadilishia taulo za kike ni changamoto nyingine kwani hutumia vyoo vya kawaida ambavyo alieleza kuwa havina maji  na ni vichafu.
Anasema kukosekana kwa maji katika vyoo kunaweza kusababisha magonjwa ya U.T.I, kuhara na hata kipindupindu.
Ruth Mzinga  ni mwalimu na  mlezi wa wasichana katika shule ya sekondari Imezu, anasema ukosefu wa maji shuleni hapo unawaathiri kwa kiasi kikubwa wanafunzi  wa kike kutokana na kuwa maumbile yao kuhitaji zaidi matumizi ya maji.
Mwalimu Mzinga anasema  ukosefu wa maji shuleni hapo pia umechangia kwa kiasi kikubwa wazazi au walezi kutowapeleka mabinti wao hosteli.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Tibus Makona  amekiri kuwepo kwa changamoto ya ukosefu wa maji na kueleza kuwa anayeathirika zaidi na kadhia hiyo ni binti.
Anasema Shule haina uwezo wa kuleta maji licha ya kuwa kuna miundo mbinu ya mabomba ambayo alisema yanatoa maji mara moja kwa mwezi au wakati mwingine kutotoka kabisa.
Inasema idadi kubwa ya wanafunzi shuleni hapo ambayo kwa sasa  imefikia wanafunzi 862 wasichana wakiwa ni 488 na wavulana 374 inatoa taswira ya uhitaji mkubwa wa maji.
Makona  ameleeza kuwa katika kumsaidia mtoto wakati wa hedhi Shule imeweka utaratibu wa kununua dazani moja ya taulo za kike kwa kila mwezi kwa kutumia fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya kununulia madawa.
Amesema taulo hizo za kike hazikidhi mahitaji kwa wanafunzi wote wenye uhitaji lakini wanamsiadia binti ambaye amepata dharula awapo shuleni.
Hata hivyo Makona amesema kuwa hosteli inauwezo wa kubeba wanafunzi 160 lakini kwa sasa ina wanafunzi 34.
Akizungumzia kadhia ya maji Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Inyala, Mwalingo Kisemba,  alisema kuwa Serikali inatambua jinsi changamoto ya maji inavyoathiri elimu ya mtoto wa kike ambapo amesema kwa  sasa wamenunua tanki ambalo litatumika kuvunia na kuhifadhia maji katika kipindi hiki cha masika.
Licha ya kuwa Serikali imetoa msaada wa  tanki la Maji shuleni hapo ambalo bado halijatengenezwa miundo mbinu kwa ajili ya kutumika watahakikisha wanafanya haraka ili kunusuru hali hiyo.
“Mtoto wa kike hushindwa kuhudhuria masomo siku tano kila mwezi kutokana na sula la hedhi na miezi miwili kila mwaka, hali hii sio nzuri kwani utoro huo usababishwa na changamoto ya kukosa taulo za kujisitiri na ukosefu wa maji pia jitihada zinahitaji ili kuwasaidia mabinti zetu hawa,” alisema Mwalingo.
Naye Ofisa Maendeleo ya Jamii halmashauri ya Mbeya, Zena Kapama alisema kuwa kwa kutambua changamoto wanazozipata watoto wa kike wawapo shuleni Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya imetenga jumla ya shilingi milioni 1.6 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya ununuzi wa tatulo za kike ambapo utekelezaji wake utazinufaisha shule za Sekondari 28 za Wilaya hiyo.
Kapama anasema wanatambua ukubwa wa tatizo kwa mabinti lakini kwa kuanzia itasaidia na kuahidi kuongeza bajeti wakati mwingine kadri fedha zitakapopatikana.
TGNP Mtandao ni taasisi inayojenga uwezo kwa wananchi kuibua suala la upatikanaji wa pedi za bure kwenye mikutano ya vijiji na mitaa na kuomba serikali za vijiji na kamati za maendeleo za Kata (WDC) kupanga kwenye bajeti zake ili shule za kata zitoe bure pedi kwa wasichana.
Hadi sasa halmashauri tatu ambazo watumishi wake wamejengewa uwezo na TGNP Mtandao zimeshapanga  fedha kwenye bajeti zake kuwezesha wasichana kupata bure pedi mashuleni. Halmashauri hizo ni Kishapu, Kisarawe na Mbeya.

Monday, May 21, 2018

Ukosefu wa maji safi na salama Kishapu unakwamisha elimu



Na  Kareny  Masasy


Tatizo la maji kwa Kishapu limeendelea kuwa kubwa licha na mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kufikia baadhi ya maeneo. 

WANANCHI  wa kijiji cha Ng’wang’hili  kata ya Bunambiyu  halmashauri ya wilaya ya Kishapu  wamelazimika kuchimba bwawa la maji  kwenye kiwanja cha shule ya msingi ya kijiji hicho ili kuweza kuvuna maji nakuondoa kero ya maji kwa wananchi na wanafunzi wawapo shuleni.

Lakini upatikanaji wa maji hayo umekuwa siyo safi na salama kwani  mazingira  yaliyopo  bwawa hilo siyo salama kwani baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo hasa darasa la awali na la kwanza  hulazimika kujisaidia  nje ya choo cha shule na kinyesi kutapakaa hovyo.

Mwalimu Faustine Kuhenga anasema kuwa bwawa hilo limechimbwa kwa nguvu za wananchi kutokana na uhaba mkubwa wa maji katika shule hii ikiwa hata jamii yenyewe  bwawa hili limekuwa likiwasaidia kwa maji ya  matumizi ya nyumbani na kunywa.
“Bwawa hili lipo katika mazingira ya shule walifanya hivyo ili kuweza kurahisisha huduma ya maji kwa wanafunzi kwaajili ya kunywa  pia jamii yenyewe imekuwa ikilitegemea bwawa kwa kuvuna maji nakuwasaidia kipindi cha kiangazi ingawa hufikia wakati hukauka pia”anasema  mwalimu Kuhenga.

Pia anasema kuwa shule hii ina matundu ya vyoo manne ambayo hutumika lakini baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakijisaidia nje ya vyoo   na msimu huu wa mvua  maji hujaa  maeneo yote  nakuchanganyikana lakini bado wanaendelea  kila siku kuwapatia elimu wanafunzi hao kmatumizi ya vyoo.

“Unafahamu  jamii  hapa kijijini bado inamwamko mdogo wa elimu  hata utunzaji wa mazingira kwa maeneo wanayotoka wanafunzi hawa vyoo vyake havina ubora  na umri wao inaonekana wanajisaidia nje ya vyoo hili tumeliona na kila siku kabla ya vipindi hutoa elimu ya  juu ya afya na matumizi ya vyoo lakini bado hawaelewi”anasema mwalimu Kuhenga.
Anasema hata uvunaji wa maji kwenye tanki lililopo husaidia kipindi cha mvua pekee na msimu wa kiangazi hakuna maji na bwawa hili husaidia hadi jamii kwa kipindi kifupi nalo hukauka na kulazimika kwenda kuyafuata maji safi na salama kwenye kijiji cha Ng’wang’osha  umbali wa kilomita  20  kwa baiskeli au wakati mwingine kwa miguu.

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho  Shija  Reuben  na  Ester Swilasi wanasema kuwa kuna shida kubwa ya maji kipindi cha kiangazi bwawa la shule  lilichimbwa ili kuvuna maji  kipindi cha masika nakuweza kuwasaidi wanafunzi hata jamii yenyewe nalo hawalitegemei sababu ni muda mfupi hukauka nakulazimika kuyafuata maji umbali wa kilomita 20  na shughuli zote za kujitafutia kipato husimama.

“Maji ya bwawa hilo sasa hivi huwezi kuona linatumiwa na jamii sababu ya mvua zinanyesha madimbwi mengi yamejaa maji mvua ikiacha kunyesha  vitongoji vyote sita hutegemea kwenye bwawa la shule hiyo kwaajili  ya kunywa na matumizi mengine ambayo siyo safi na salama isitoshe jamii nayo imekuwa ikijisaidia hovyo kwa kukosa  vyoo  ambavyo vimetitia kwa sababu ya mvua.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Buzali Mabele anasema kuwa  kweli kuna shida ya maji  kwenye kijiji hicho kilicho na vitongoji sita ambavyo ni mwamatembe,Mwasegagi,Mwakajala,Igunagahabi,Mwanjige na Mwamajigi nakutegemea bwawa la shule walililichimba hivi sasa huwezi kuona kama wanalihitaji sababu wanachota kwenye madimbwi mengine yaliyo na maji msimu huu wa mvua.
“Lakini  yakikauka  maji ya kwenye madimbwi  hulazimika kuchota  maji ya bwawa la shule  pia ukosefu wa vyoo katika kaya kujisaidia vichakani naona ni muda huu wa mvua kwani walikuwa na vyoo ingawa vilikuwa havina ubora vimetitia sababu ya mvua kubwa kunyesha na ardhi ilivyo ya kijijini hapo”anasema  Mabele.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Emanuel  Magesa anasema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1981 na mpaka sasa ina jumla ya wanafunzi 480  wa darasa la awali  pekee ni 90  na  darasa la  kwanza ni 112 ambao ni wengi na umri wao  ni mdogo bado hawajafahamu matumizi ya matundu ya vyoo hata katika mazingira wanayotokea ndani ya familia zao hilo limekuwa changamoto  hali iliyopo wamekuwa wakijisaidia nje ya matundu ya vyoo  na katika mazingira ya shule ikiwa kuna bwawa la maji ambapo wamekuwa wakielimishwa.
Mtendaji  wa kijiji hicho  Thomas  Nyonyo anasema kuwa   bwawa la shule lilichimbwa kwa nguvu za wananchi baada ya kupata mradi wa lishe shuleni uliotolewa na shirika  la lishe  mwaka 2015 ambapo wanafunzi walihitajika kupata chakula kilichokuwa kikipikwa shuleni hapo na kuwepo uhaba mkubwa wa maji.
Nyonyo anasema  bwawa hilo limeweza kuwasaidia  wanafunzi kupata maji ya kunywa na jamii  ingawa kwa muda mfupi kwani  wanalazimika kuyafuata maji umbali wa kilomita 20 halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  kata ya Iselamagazi  kijiji cha Ng’wang’osha.
Pia anasema wakitaka kufuata maji katika kijiji cha Bunambiyu kuliko na bomba la maji safi na salama  ni umbali  wa kilomita 15 kuyapata hivyo  kwa wastani kijiji chote hakina maji zaidi yakutegemea  bwawa lililopo shuleni ambapo maji yake nayo yanaonekana siyo safi na salama kutokana na mazingira yake.
“Bwawa hilo lililopo shuleni linahitaji utunzwaji na usimamizi mzuri ili kuepuka mlipuko wa magonjwa  katika jamii kwani hata upande wa jamii yenyewe umekuwa hauna vyoo bora  hivi sasa kipindi cha mvua  karibu vyoo vingi  kwenye kaya vimetitia nakufanya kujisaidia vichakani hovyo kikiwepo cha shule chenye matundu mawili nacho kimetitia pia”anasema  mtendaji wa kijiji Nyonyo.
Anasema mpango uliopo  ili kuweza kupata  maji safi na salama  ya kunywa  waliitisha kikao cha kijiji nakufikia maazimio ya kila kaya kuchangia kiasi cha shilingi 50,000 ili kuyavuta bomba la  maji kutoka kijiji cha Bunambiyu  nakuweza kupata maji safi na salama  na wananchi wamedai wako tayari wakati watakapo uza mazao yao ikiwa kijiji  hicho kina kaya 218 na idadi ya watu 1882.
Diwani wa kata ya Bunambiyu Richard Sangisangi anasema kuwa  kijiji hicho kweli hakina bomba kina shida ya maji  nani umbali mrefu kuyafuata maji kwani hata haya yaliyopo hayatoshelezi kwa idadi ya watu waliopo  kwenye kata nzima  hata miundombinu ya bomba hilo sio imara  limekuwa likihalibika  mara kwa mara.
Mganga msaidizi wa kituo cha afya Bunambiyu   Simba Rajabu anasema kuwa idadi kubwa ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa kituoni hapo huja na magonjwa ya kuhara  idadi kubwa ni watoto  sababu ni kutokana na mazingira wanayoishi  nakutumia maji yasiyo safi na salama .
Dkt Rajabu anasema kuwa mara kwa mara wamekuwa wakiwapatia elimu juu ya afya zao na mazingira wanayoishi ya ukosefu wa matundu ya vyoo au kuwa na vyoo bora  kwani upande wa  huduma za maji ni shida kwao hupata maji yasiyo safi na salama  katika vyanzo vya maji na hawana desturi ya kuyachemsha ili kuua wadudu matokeo yake  kupatwa na magonjwa ya mlipuko kama kuhara walio wengi.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Stephen Magoiga  anasema kuwa kijiji hicho siyo pekee kuwa na changamoto ya  kukosa maji ni vijiji vingi hilo  linaeleweka  ila mpango uliopo  mradi wa  maji ya ziwa Victoria umeanza kuenea maeneo mengi jitihada zitafanyika kuvuta mabomba ili kuwarahisishia wananchi huduma yakupata maji karibu kwa mujibu wa sera ya maji  nakuondokana na kutafuta maji umbali mrefu.
Anasema  lipo suala la  jamii kukosa vyoo vyenye ubora  na msimu wa mvua kweli vimetitia  na matokeo yake baadhi  yao kuendelea kujisaidia vichakani  bila ya kujenga wanaweza kueta athari kwenye vyanzo vyao vya maji   lakini bado wanaendelea kila siku kuwapatia elimu juu ya utunzaji mazingira nakujenga vyoo vyenye ubora  ili kuepuka mlipuko wa magonjwa kama kipindupindu na kuhara.
Halmashauri ya wilaya ya Kishapu ni miongoni mwa maeneo hapa nchini ni  kame  yasiyopata mvua za kutosha  ambapo asilimia 88 ya wakazi wake ni wafugaji na wakulima na  asilimia 27 ni wakulima pekee.
Hata hivyo Sera ya maji ya mwaka  2002 inaeleza kuwa uvunaji wa maji ya mvua  ni njia  muhimu yakupata  maji hususani katika maeneo kame ambako yanaweza kuwa ndio chanzo pekee cha maji  cha kuaminika  katika kipindi cha msimu wa kiangazi.
Pia moja ya uvunaji ya maji  wananchi  wanaoishi vijijini watahamasishwa  kutumia teknolojia  hii ikiwa ukosefu  wa maji safi na salama  na kutofuata  kanuni bora za afya  na usafi wa mazingira  ni  chanzo kikubwa  cha mlipuko wa magonjwa  na vifo  na husababisha wimbi la umasikini  hasa kwa wanawake na watoto.
Hata hivyo sera hiyo inaeleza kuwa ili kuboresha  afya ya jamii mkazo utawekwa  kwenye mipango ya pamoja  inayojumuisha  utoaji wa huduma  za maji,usafi wa mazingira  na elimu ya afya .

MWAMKO MDOGO WA ELIMU KWA WAZAZI UMEFANYA KUTOTHAMNI ELIMU KWA MTOTO.


Na  Kareny  Masasy, Kishapu

MWAMKO  mdogo wa elimu  kwa wazazi wa  kata   ya Bunambiyu halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  imebainika  kuwarudisha nyumba maendeleo ya watoto wao kielimu kwa kuthamini  kuwatumikisha kazi za shambani  na kuchunga mifugo.
Licha ya hali hiyo pia wamekuwa wakiwaeleza wanafunzi wa kike  wafanye vibaya katika mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi ili wasifaulu  na baadaye waolewe lengo la mzazi kupata utajiri wa ng’ombe.
Mwalimu  mkuu wa shule ya msingi Ng’wang’hili  iliyopo kijiji hicho  Emmanuel  Magesa anasema kuwa  kumekuwepo na mdodoko  wa wanafunzi kushindwa kumaliza shule  kwasababu yakupewa majukumu ya kuchunga mifugo.
Hata hivyo anasema kuwa  hali hiyo inasababishwa na  baadhi ya wazazi kuwa na mwamko mdogo wa elimu ambapo changamoto nyingine  wamekuwa wakihamisha watoto wao bila kutoa taarifa yoyote.
“Anasema mfano  waliopo darasa la saba sasa hivi walianza darasa la kwanza mwaka 2012  wakiwa 51 ambapo  wavulana ni  22 na wasichana ni 29  na  hadi leo hii  kuna wanafunzi 19 tu ambao wanatarajia kufanya mtihani wasichana 8 na wavulana 11”anasema  mwalimu mkuu wa shule hiyo..
Mwalimu Magesa anasema kuwa  mafanikio ya elimu bure  yamefanya uandikishaji  wa wanafunzi  wa darasa la kwanza kutoka wanafunzi  50 kwa miaka ya nyuma  hadi kufikia  wanafunzi 112 kwa sasa.
Pia  uandikishaji   wa darasa la awali  ulikuwa wanafunzi 25  zamani hadi  kufikia 100 ambapo idadi inaanza kupungua  taratibu pindi wanapoanza kuingia darasa la  tano hadi la saba sababu wameonekana kukua kwa kutumikishwa kazi za shambani na kuchunga mifugo.
Magesa anasema kumekuwepo na baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaeleza watoto wao wafanye vibaya siku ya mtihani  wakumaliza elimu ya msingi katika hali ya matokeo kuanzia mwaka 2015 shule hiyo  walimaliza wanafunzi  22 na wawili tu ndio waliofaulu kuendelea na elimu ya masomo ya sekondari.
Pia mwaka 2016  wanafunzi  waliofanya mtihani darasa la saba walikuwa 21 ambapo wavulana  ni tisa na wasichana 12 na wote walifaulu ikiwa mwaka 2017 waliofanya mtihani ni 19  na nane  hawakufaulu ambao wavulana ni watatu na wasichana ni watano.
Anasema  licha yakuwepo utoro wa rejareja unaosababishwa na miundombinu mibovu hasa kipindi cha masika ambapo darasa la awali na darasa la kwanza hawaji shule  na hata ukimrudisha mwanafunzi amfuate mzazi wake aje mzungumze ndio umempatia  unafuu wa mwanafunzi kuendelea kukaa nyumbani na mzazi haji.
Mwanafunzi wa shule ya  msingi Ng'wang'hili  kata ya Bunambiyu aliyeacha shule  akiwa darasa la tano  nakuendelea kuchunga mifugo ya wazazi wake.  Picha na Kareny  Masasy.

Baadhi ya wazazi wa kata ya Bunambiyu   Modesta Obedi na Ernest Hausa wanasema kuwa wazazi wamekuwa wakishikwa na tamaa ya kupata utajiri wa ng’ombe kwani wamekuwa wakiwaeleza wanafunzi wa kike kufanya vibaya katika mitihani yao ya mwisho ili waweze kuolewa na mzazi kumiliki ng’ombe jambo ambalo anaona ni ufahari kwake.
Ernest Hausa anasema kuwa  kweli wapo wazazi wanaowatumikisha wanafunzi kazi za shambani msimu wa kilimo anaona wanao uwezo wa kulima msimu wa mvua umefika hakuna nguvu kazi bora aende akamuombee ruhusa shuleni kwa kusema uongo  nakumtumikisha  kuliko apate elimu.
Licha ya suala la  uchungaji mifugo  pia anasema  huwatumikisha shambani kwaajili yakulima vibarua  kwenye shamba la mtu nakupata fedha za  chakula msimu wa mvua  za masika kipindi cha kilimo.
 Mwenyekiti wa kijiji  cha  Ngw’ang’hi  Buzali Mabele anasema kuwa  wazazi wamekuwa wakiwaachisha shule watoto wao ili kuchunga mifugo na kulima au kuhama bila kutoa taarifa na kuwaozesha umri mdogo  hilo sasa limeingizwa kwenye mpango mkakati wa kijiji kuzibiti hali hiyo  isiendelee kwa kuwachukulia hatua za kisheria.
Mtendaji wa kijiji  cha   hicho  Thomas  Nyonyo anasema kuwa hivi sasa wameanza kuzibiti utoro kwa  kuwasaka wazazi ambao wanahama kimya kimya  na watoto wao ambao wanasoma shule  na kuwaeleza kuacha tabia ya kuwarubuni wafanye vibaya kwenye mitihani yao yakumaliza elimu ya msingi.
Wengine wazazi wamekuwa wakiwatumikisha shughuli za  shambani na kuchunga mifugo kwa kuona kwenda shule ni kero kubwa kwani idadi kubwa ya wazazi hawajasoma isitoshe ni jamii ya wafugaji  hasa  wanaoishi katika kijiji  utakuta mwenye ng’ombe chache ni 50.
Diwani wa kata ya Bunambiyu  Richard Sangisangi anasema kuwa kweli wazazi bado wanamwamko mdogo wa elimu wamekuwa  wakiwaachisha watoto wao kwenda shule ili wafanye kazi za shambani au kuchunga mifugo hilo limepigwa marufuku atakaye  bainika  mzazi atachukuliwa hatua na miundomibu ya barabara  msimu wa mvua unachangia utoro wa rejareja kwa wanafunzi.
Mkuu  wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba anasema kuwa  suala la wazazi wafugaji kutoruhusu watoto wao kwenda shule  hilo lipo ila walikuwa wakielezwa umuhimu wa elimu na kuwachukulia hatua wazazi watakao bainika kufanya kitendo hicho.
Hata hivyo Talaba anasema kuwa tayari yamekwisha tolewa maagizo  kwa  watendaji wa vijiji na kata kufuatilia wanafunzi watakao  watoro wanaosababishwa na kutumikishwa kazi mashambani na kuchunga mifugo ili wazazi waweze kuchukuliwa hatua  za kisheria.
“Kweli jamii ya wafugaji watoto wao wamekuwa hawasomi na wilaya hii asilimia 88 ni wafugaji na wakulima  ndio wanategemea kwa kuwainulia kipato lakini tabia ya kutowaombea  uhamisho shuleni  ipo, hata ukitaka kuwachukulia hatua wazazi unashindwa  utawapatia wapi?”alisema  mkuu wa wilaya.
Mkurugenzi Mtendaji  halmashauri  ya Kishapu Stephen Magoiga anasema kuwa  baadhi ya wazazi wamekuwa wakienda shuleni kuwaombea ruhusa watoto wao wanaumwa kumbe ni uongo wamekuwa wakifanya hivyo lengo kuwapeleka shambani kulima au kulichunga mifugo.
“Kuna mzazi mmoja tulielezwa amemuombea ruhusa mwanaye kuwa anaumwa lakini tulifuatilia mpaka shambani alipoenda yeye na mwanaye tukamkuta shambani mzazi huyo alichukuliwa hatua lakini aliomba msamaha kuwa  hatorudia tena  tena  ambapo ndio imekuwa tabia ya  baadi yao wazazi”alisema mkurugenzi.
Hata hivyo mkurugenzi Magoiga anasema kuwa kuna shule  za msingi 117  ambazo baadhi yao  maeneo yalipo  wanafunzi kweli wanalazimika kutembea umbali mrefu  hasa kijiji ch Ng’wang’hili  vitongoji vyake viko mbalimbali kwani wanafunzi wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita  zaidi ya saba kwenda shule nalo linasababisha utoro au kuacha shule.
Anasema  halmashauri hiyo matokeo ya darasa la saba kwa mwaka jana walishika nafasi ya mwisho kimkoa  katika halmshauri sita zilizopo hivyo ni jitihada zinahitajika baada ya kuweka mkakati kwa mwaka huu  kwa mwalimu mkuu  ambaye shule yake ikifelisha idadi kubwa  ataondolewa kwenye nafasi hiyo.
 Katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania  ya mwaka 1977 inaeleza kuwa  mtoto anahaki  ya kulindwa na kupendwa ,anayo haki ya  kupata elimu,kucheza na kujieleza  pia serikali imekomesha utumikishwaji wa watoto mashambani wala katika biashara ndogondogo

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bunambiu Kishapu wanakaa chini

Wanafunzi wa Kidato cha kwanza shule ya sekondari Bunambiu wakiwa kwenye darasa ambalo limejaa na madawati hayatoshi

 wasichana wakiwa wamekaa chini wakijisomea, hili ni moja wapo ya darasa ambalo halina madawati kabisa na wasichana wamekuwa wakipata shida kujisitiri kutokana na ukosefu wa madawati shuleni.

Tuesday, April 17, 2018

WANAKIJIJI WALILIA KITUO CHA AFYA KATA YA ITEWE MBEYA



SERA ya afya ya mwaka 2007 imeelekeza kuwa kila kata inatakikwa kuwa na kituo cha afya na kila kijiji kuwa na Zahanati ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa wanaoishi maeneo ya pembezoni.
Mkakati wa kufikia lengo la sera hiyo ni Serikali kushirikiana na wananchi pamoja na wadau wengine ambapo pia serikali inatakiwa kuhakikisha kunakuwepo na watoa huduma wa kutosha, vifaa tiba na dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya.
Pia sera hiyo imesisitiza namna  Serikali itakaposhirikiana na wadau na wananchi katika juhudi za kupanua na kukarabati majengo ya kutolea huduma za afya pamoja na kuhakikisha kunakuwepo na  uwiano wa kijiografia katika kutoa huduma za afya nchini.
Utekelezwaji wa sera hiyo katika maeneo mengi hasa ya pembezoni mwa miji bado haujafanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na kuwepo kwa changamoto lukuki za upatikanaji wa huduma za afya.
Miongoni mwa sehemu ambazo hazijaguswa na Tamko la Sera hiyo ni kata ya Itewe iliyopo katika halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, ambayo ilianzishwa mwaka 2009, kutoka kwenye kata mama ya Iyela.
Kata ya Itewe ni Miongoni mwa kata 28 za halmashauri ya Mbeya vijijini ikiwa  ina jumla ya watu 4655, kaya 1108 na ina jumla ya vijiji vitano ambavyo ni Iyela-Nyara, Idunda, Tembela, Itewe na Isongwa.
Licha ya kata hiyo kuhudumia vijiji vitano lakini hadi sasa haina kituo cha afya na wananchi wake wanategemea kupata huduma katika zahanati moja tu ambayo ipo katika kijiji cha Idunda jambo ambalo linaathiri kuzorota kwa huduma ya afya katika kata hiyo.
Hata hivyo zahanati hiyo haina Miundombinu ambayo inakidhi mahitaji ya wagonjwa hasa akina mama wajawazito kwani ina vitanda viwili tu, ambapo kati yake kimoja kinatumika kwa ajili ya kujifungulia na kingine kwa ajili ya kupumzika.
Wanananchi hasa wanawake wanaoishi katika kata hiyo wanapaza sauti zao kwa kuiomba serikali kuwajengea kituo cha afya au kuboresha miundombinu ya zahanati hiyo ili waondokane na adha ya kutopata huduma bora za afya.
Wanawake hao walitumia mbinu ya igizo kufikisha kilio chao Mbele ya viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Mbeya ili waione changamoto yao, waichambue na kuifanyia utekelezaji kwa lengo la kuboresha huduma za afya katika kata yao hasa kwa mama na mtoto.
Kupitia igizo hilo walionesha namna akina mama wajawazito wanavyokuwa wanajifungulia njiani kutokana na kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya hadi katika zahanati ya kijiji cha Idunda ambayo inahudumia kata nzima kutokana na kukosekana kwa kituo cha afya.
Pili Daniel, mkazi wa Itewe yeye aliigiza kama mama mjamzito akionesha uhalisia wa mazingira yao ambapo alionesha namna wanawake wajawazito wanavyojifungua njiani na wakati mwingine wanavyotozwa faini ya 10,000 na wahudumu wa afya kwa kosa la kujifungua njiani ama nyumbani.
Kupitia igizo hilo anasema umbali mrefu umekuwa ukisabaisha wanawake wa kata hiyo kujifungulia nyumbani au njiani au wakifika kwenye zahanati wanakosa sehemu ya kupumzikia kutokana na kukosekana kwa kitanda.
“Huko zahanati hata maji hakuna, tunatumia ya mtoni, wakati mwingine nesi anaenda kuchota au sisi wenyewe tunaenda mtoni kuchota ili yatusaidie wakati wa kujifungua,” alisema
Igizo hilo limebeba uhalisia wa maisha wanayopitia wananchi wa kata hiyo hasa wanawake, ambapo mkazi wa kata hiyo Wilbroa Ndezi ameongezea kwa kusema kuwa wakati mwingine wamekuwa wakikosa dawa wanapokuwa wamefika kwenye zahanati hiyo kwa ajili ya kupata matibabu jambo ambalo linapelekea waende kununua kwenye maduka ya watu binafsi kwa gharama kubwa.
Amesema licha ya kukata bima ya afya kupitia mfuko wa bima ya afya ya Taifa (CHF) kwa gharama ya sh.12,000 kwa mwaka au sh.6000 kwa  mtu mmoja bado wamekuwa wakikosa baadhi ya dawa.
“Kuna wakati unaona ni heri usiende zahanati, kule unaweza kufika ukaelezwa kuwa dawa hamna nenda kanunue kwenye duka la madawa la watu binafsi wakati wale wanaokuja kuandikisha bima walitueleza kila kitu tutakipata pale zahanati,” alisema.
Edda Mwalima amesema kuna wakati mama mjamzito akifika katika zahanati hiyo au Mgonjwa wa kawaida anakaa muda mrefu kusubiri huduma kutokana na uhaba wa watumishi na wakati mwingine anarudu nyumbani bila kupata huduma.
Amesema kukosekana kwa vitanda vya kupumzika kumekuwa kukisababisha baadhi ya wanawake wajawazito kutoona umuhimu wa kwenda zahanati na kuamua kujifungulia nyumbani jambo ambalo si salama kwa afya zao na watoto wao.
Kaimu Ofisa Mtendaji wa kata hiyo Michael mwaifweya anakiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kueleza kuwa wameanza kujenga miundombinu Majengo kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa utoaji huduma katika zahanati hiyo.
Amesema majengo hayo yanajengwa kwa nguvu za wananchi na kwamba yakikamilika yataondoa kero zilizopo na kuwa sasa wanatafuta eneo ambalo litajengwa kituo cha afya cha kata.
Mganga mkuu wa Zahanati hiyo, Angel Mabula amesema zahanati hiyo inawahudumu watatu na kwamba wanakidhi mahitaji ya wagonjwa kwa kuwa idadi ya wagonjwa wanaofika kupata huduma ya afya kwa siku ni wachache.
Amesema kwa siku wanawahudumia wagonjwa kwa wastani wa watu 5 hadi 3 na wakati mwingine 10 hadi 15  kulingana na majira ya hali ya hewa ambapo kwa wastani wa mwezi mmoja wajawazito 10 wanafika kliniki kwa ajili ya kufuatilia maendeleo ya mtoto.
“Kwa siku anaweza kuja mjamzito mmoja  hadi sita, lakini kwa watani wajawazito 100 wanafika kwa mwaka kuhudhuria kliniki, hapa kwenye zahanati kwa kweli hakuna msongamano wa wagonjwa licha ya kuwa kata ina zahanati moja, kwa sababu tumeweza kutoa elimu ya namna ya kuepukana na magonjwa yanayoweza kuzuilika na wagonjwa wengine wanaenda kituo cha afya Inyala,” amesema
Amesema kwenye chumba cha kujifungulia (Labour room) kuna vitanda viwili ambapo kimoja kinatumika kwa ajili ya kujifungulia na kingine kwa ajili ya kupumzika hivyo inapotokea wamepokea wagonjwa wengi inakuwa ni vigumu kuwamudu hivyo wengine wanalazimika kupumzika kwenye kitanda cha wagonjwa wa kawaida ambacho kipo kimoja.
Amesema kwa kuwa vijiji vingi vipo mbali na zahanati wakati mwingine wanalazimika kufanya kazi nje ya kituo kwa kuwafuata wananchi na kutoa huduma za kuwapima watoto na wanawake wajawazito na kwamba wameagiza kila kijiji kinunue kitanda na godoro kwa ajili ya kupumzikia wagonjwa.
Amebainisha kuwa kwa takwimu za mwaka 2017 wajawazito 48 walijifungulia kituoni hapo wakati tisa wakijifungulia njiani ama nyumbani ambapo kwa mwaka huo kiliripotiwa kifo cha mwanamke mmoja ambaye alijifungulia nyumbani.
“ Mwaka jana watoto sita chini ya umri wa mwezi mmoja walifariki dunia katika jamii hii,chini ya mwaka mmoja kifo kilikuwa kimoja na chini ya miaka mitano vifo vilikuwa n inane,” alisema
Amesema dawa zote muhimu zipo za kutosha katika zahanati hiyo na wakati mwingine zinapita muda wake wa matumizi (expire date) kutokana na idadi ndogo ya wagonjwa wanaofika katka zahanati hiyo.
Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Zena Kapama amesema serikali inatatua changamoto za wananchi kutokana na kipaumbele chao walichokiibua kupitia mikutano yao na kamati ya maendeleo ya kata (WDC) na kuwasilishwa kwenye halmashauri.
Amesema kwa sasa wananchi wanapaswa kuibua mradi kulingana na huduma wanayohitaji na kuanza kuitekeleza na serikal jukumu lake ni kumalizia na kuleta watumishi kwa ajili ya kutoa huduma na kwamba suala la afya si kipaumbele kwa sasa kwani halijaletwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19.
Hata hivyo serikali mkoani Mbeya imeanza mikakati maalumu ya kuimarisha afya ya msingi kwa wananchi ili kuimarisha nguvu kazi kwa ajili ya shughuli za kijamii na kiuchumi  ikiwemo ujenzi wa Viwanda na shughuli za kilimo.
Moja ya mikakati iliyoanzishwa na Serikali hiyo ni Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla, kuwafunga vitanzi wakuu wa Wilaya zote za Mkoa huo kwa kuwasainisha Mkataba maalumu wa uhamasishaji wa ujenzi wa vituo vya Afya kwenye kila Kata, ujenzi wa Zahanati kila kijiji na kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Mkataba kama huo ulisainiwa kati ya Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Nyasebwa Chimagu na wakurugenzi watendaji wa Halmashauri zote za Mkoa huo.
Akizungumza na wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wa Halmashauri zote, Waganga wakuu wa Wilaya na maofisa watendaji wa Kata zote za Mkoa wa Mbeya , Makalla amesema mkataba huo unawasisitiza viongozi hao kwenda kuwahamasisha wananchi kujenga maboma ya vituo vya Afya kwenye Kata zao na Zahanati kwenye vijiji ili Serikali imalizie kwenye uezekaji.
Amesema Mkoa wa Mbeya una jumla ya Kata 178 lakini zenye vituo vya Afya ni 25 pekee, huku vijiji 300 kati ya 533 ndio vikiwa havina zahanati kama inavyotakiwa.
“Hatuwezi tukawa tunasema Hapa kazi tu! Na kusisitiza uchumi wa viwanda wakati wananchi wetu hawana uhakika wa kupata huduma za afya jirani na maeneo yao, hivyo Mkataba huu utamlazimisha kila mtu kuhakikisha tunaimarisha afya za watu wetu,” amesema Makalla.
Hata hivyo amesema ili kuweka msisitizo wa Mkataba huo nakala zake atazituma kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa, Sulemani Jafo na Makatibu wakuu wa Wizara hizo.
Makala amesema watahakikisha wanahamasisha wananchi kwa kuanzia na viongozi wao ili mpaka kufikia mwaka 2020 kila kijiji kiwe tayari kina Zahanati, kila Kata iwe na Kituo cha Afya na asilimia 100 ya wananchi wawe wamejiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Mwisho.

Monday, April 16, 2018

serikali itenge bajeti ya wananchi kuondoa mzigo wa kazi kwa wanawake wa vijijini

Kituo cha Taarifa na Maarifa Ukenyenge wakikabidhi mchango wa fedha kwa viongozi wa Gender Club ya shule ya sekondari Ukenyenge kwaajili ya kununualia mahitaji muhimu kwa wasichana.
 Hali halisi ya upatikanaji wa maji katika Halmashauri ya Kishapu ni changamoto hasa kwa wanawake na watoto. muda mwingi unatumika na wanawake kutafuta maji badala ya kufanya shughuli za Maendeleo hasa uchumi.

Thursday, March 15, 2018

Free pads help girls excel in education


 Kishapu District Council Head of Community Development, Mr. Joseph Swalala receiving award from Her Excellency Vice President Samia Suluhu, During the 13rd Gender Festival at TGNP Mtandao September 2017



Kisarawe District Council Vice Chair Person Ms. Amina Lilomo, receiving award  on behalf of Council for budgeting for free sanitary pads to secondary school girls 

Free pads help girls excel in education

By Deogratius Temba

Neema Joseph is among the happiest students who sat for their ordinary level national examinations at Ukenyenge ward Secondary School in Kishapu District Council, Shinyanga region November 2017.

The reason for her contentment is non-other-than her results which enabled her to score division two, thus automatically booking a chance to join advanced level education at any government-run school later this year.

Neema plus other two girls of that same school managed to score that high competent pass, despite the fact that their school was facing a number of challenges, including enough books, teachers and laboratories.

She admits that she was able to attend all class periods while in form four, because the district authorities had set aside a budget to buy them sanitary kits which enabled them get enough pads to use during their normal monthly menstruation circles.

“I should admit that I used to excuse myself from school during this particular time of the month, because at times I did not have enough sanitary towels to help me, so remaining at home was the only option. I thank all that have collaborated in helping us” says Neema who is eagerly waiting to join form five later this year.

Neema’s bliss is supported by Ms. Fredina Saidi, who is Ukenyenge Secondary School Board Chairperson, who says that since that school started providing free pads to girls, the attendance has doubled, and academic performance for girls has also increased tremendously.

She says that in the past, boys in the same school used to insult girls while on menstruation, but since they were educated on the biological situation of their sisters, they have appreciated and stopped to shaggy dog them.

According to Fredina, Ukenyenge Secondary school had one pit latrine with only one latrine for girls, but today, the same school has 12 latrines which can serve all the girls without problems, and there is enough water for their cleanliness.

This school has succeeded in this program aimed at providing free pads to girls, thanks to tireless efforts put forward by Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) that has organized some Gender Responsive Budgeting training 8 district executives from Kishapu, Kisarawe, Mbeya, Tarime, Morogoro, Ilala, Kinondoni and Temeke districts Councils. After the GRB training held in December 2016, only Kishapu and Kisarawe managed to allocate fund to provide free sanitary pads to secondary school girls. Kisarawe. The Kishapu targets were to support 256 secondary girls with sanitary materials by June 2018. (Kishapu Budget Book 2017/18; pg 90)

Joseph Swalala who is Kishapu District Head of Community Development department admits that girls’ school attendance has improved and there is academic competitiveness among boys and girls.

“This hygienic improvement for girls is not only implemented at Ukenyenge School but we are planning to do the same thing to all the schools in our district. We have set a 5 per cent of our budget in 2018/2019 FY for this particular purpose” says Swalala.

The same views are shared by Juma Chichibera who works as Head of Kisarawe District Community Development Office, who says that there is a plan now to make sure that all girls in Ward schools are provided with enough free  pads every month.

TGNP Executive Director Ms Lilian Liundi said that girls fail to attend classes during menstrual period in some schools countrywide, and that calls for mechanisms in place to enable them feel comfortable while they are in their ‘period’.

She adds that TGNP has established Knowledge Centers across the country to give grassroots women and men access to knowledge, especially Information Communication and Technology (ICT). Also Knowledge Centers push the Local Government allocate resources for free pads, toilets latrines, safe and clean water, and reproductive health.

“At these centers men and women learn about ICT and use the facilities available to self-organize or become more involved in gender advocacy in the country” she says.

Knowledge Centers allow grassroots activists to create a bigger, more active and more powerful network for action on gender issues and other community challenges impacting upon women in Tanzania.

Currently, women account for one third of the Members in Tanzania’s National Assembly, making it one of the global leaders in women’s representation.

According to Ms. Liundi, TGNP would like to work closely with the Tanzania Women’s Parliamentary Group, a women’s parliamentary caucus on advancing gender equality through the work of the National Assembly.

As part of this partnership, TGNP is planning to organize some events in Dodoma to develop a mentorship programme for women MPs and also calls for a parliamentary seminar on implementing the program aimed at providing pads for free to all girls studying in secondary schools countrywide.

TGNP also considers mentoring as an effective way to build capacity through the support of more experienced women MPs and collaborate with people like Sauda Kilumanga who have special interest in girls’ menstrual hygiene.

TGNP sees the need to support women parliamentarians in developing their own network and in strengthening their knowledge and skills as MPs in their particular area of presentation.

When officiating at the TGNP organised 14th Gender Festival week in September last year, Vice President Mama Samia Suluhu Hassan congratulated TGNP because it helps the government offers solutions to some gender-related challenges.
 
She advised women and other organisations to change their tactics and start citing problems and providing solutions for the betterment of the people, especially the marginalised.
 
Last year, Kishapu and Kisarawe district councils were awarded for setting aside five per cent of their respective earnings for purchasing pads for school girls.

In Tanzania, as it is in most African countries, inaccessibility of sanitary towels - an important product to women and girls is one of the things that widen the gender gap.

On top of the distress of having no sanitary towels, women have to go through the ordeal of the agonizing pain that comes with the monthly flow.  

According to United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO), one in 10 African teenage girls in remote areas miss school during their menstruation cycle and eventually drop out because of menstruation related issues.

In November last year, Prime Minister Kassim Majaliwa said that the issue of sanitary pads policy among girl-student in primary and secondary schools was discussable. He was responding to a question by Catherine Ruge, Special Seats Legislator (Chadema) during an impromptu question to the Premier.

The MP had argued that the 2014 education policy requires students to study under improved environment disregard their gender, but research suggests that girls do not attend schools for three day or more due to their biological nature.

“I want to understand, there are many girls who do not have enough money to buy sanitary pads, why don’t the government come up with a policy to provide them free?” she questioned.

Majaliwa said the government wants all students to study hard and the Ministry of Health has been working to ensure that girls participate fully in education, promising that the government is ready to come up with a policy that would see girls supported.
 
In some parts of the country today, affordable sanitary protection is not easy to access, plus the social taboos related to menstruation and the culture of silence that surrounds it.

Schoolgirls in the neighbouring Kenya have started to get free sanitary pads from government since June last year.
 
The move has improved access to education in that country where many cannot afford sanitary products like pads and tampons.

The amendment to the education act, signed into law by President Uhuru Kenyatta last year stated that "free, sufficient and quality sanitary towels" must be provided to every girl registered at school, as well as providing "a safe and environmental sound mechanism for disposal".

It comes more than a decade after Kenya scrapped taxes on sanitary products in an effort to make them more affordable.
 
The move to legislate the provision of sanitary towels to school-going adolescent girls was well received by many Kenyans.

Since 2011, the Kenyan government started setting aside funds to buy and distribute the commodity to girls from disadvantaged backgrounds.

In the 2017-2018 financial year, 5 million US dollars was budgeted for that purpose. School management teams in Kenya are charged with the responsibility of purchasing and distributing the towels.
 
Experts say there’s often minimal sanitation and low levels of hygiene in such settlements, as they are overcrowded and lack formal infrastructure.
 
All in all, Tanzania urgently needs proper policies about menstruation and sanitary towels that will help the country’s girls and young women and the country should start looking at low-cost local production methods for these sanitary towels.

It would therefore sound great when the next year’s education budget is prepared, to let policymakers and education practitioners push for a special fund that will support nationwide free sanitary towels. 

 ENDS.