Na Kareny
Masasy
Tatizo la maji kwa Kishapu limeendelea kuwa kubwa licha na mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kufikia baadhi ya maeneo. |
WANANCHI wa kijiji cha Ng’wang’hili kata ya Bunambiyu halmashauri ya wilaya ya Kishapu wamelazimika kuchimba bwawa la maji kwenye kiwanja cha shule ya msingi ya kijiji
hicho ili kuweza kuvuna maji nakuondoa kero ya maji kwa wananchi na wanafunzi
wawapo shuleni.
Lakini
upatikanaji wa maji hayo umekuwa siyo safi na salama kwani mazingira
yaliyopo bwawa hilo siyo salama
kwani baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo hasa darasa la awali na la kwanza hulazimika kujisaidia nje ya choo cha shule na kinyesi kutapakaa
hovyo.
Mwalimu
Faustine Kuhenga anasema kuwa bwawa hilo limechimbwa kwa nguvu za wananchi
kutokana na uhaba mkubwa wa maji katika shule hii ikiwa hata jamii yenyewe bwawa hili limekuwa likiwasaidia kwa maji
ya matumizi ya nyumbani na kunywa.
“Bwawa hili
lipo katika mazingira ya shule walifanya hivyo ili kuweza kurahisisha huduma ya
maji kwa wanafunzi kwaajili ya kunywa
pia jamii yenyewe imekuwa ikilitegemea bwawa kwa kuvuna maji
nakuwasaidia kipindi cha kiangazi ingawa hufikia wakati hukauka
pia”anasema mwalimu Kuhenga.
Pia anasema
kuwa shule hii ina matundu ya vyoo manne ambayo hutumika lakini baadhi ya
wanafunzi wamekuwa wakijisaidia nje ya vyoo
na msimu huu wa mvua maji
hujaa maeneo yote nakuchanganyikana lakini bado
wanaendelea kila siku kuwapatia elimu
wanafunzi hao kmatumizi ya vyoo.
“Unafahamu jamii
hapa kijijini bado inamwamko mdogo wa elimu hata utunzaji wa mazingira kwa maeneo
wanayotoka wanafunzi hawa vyoo vyake havina ubora na umri wao inaonekana wanajisaidia nje ya
vyoo hili tumeliona na kila siku kabla ya vipindi hutoa elimu ya juu ya afya na matumizi ya vyoo lakini bado
hawaelewi”anasema mwalimu Kuhenga.
Anasema hata
uvunaji wa maji kwenye tanki lililopo husaidia kipindi cha mvua pekee na msimu
wa kiangazi hakuna maji na bwawa hili husaidia hadi jamii kwa kipindi kifupi
nalo hukauka na kulazimika kwenda kuyafuata maji safi na salama kwenye kijiji
cha Ng’wang’osha umbali wa kilomita 20 kwa
baiskeli au wakati mwingine kwa miguu.
Baadhi ya
wananchi wa kijiji hicho Shija Reuben
na Ester Swilasi wanasema kuwa
kuna shida kubwa ya maji kipindi cha kiangazi bwawa la shule lilichimbwa ili kuvuna maji kipindi cha masika nakuweza kuwasaidi
wanafunzi hata jamii yenyewe nalo hawalitegemei sababu ni muda mfupi hukauka
nakulazimika kuyafuata maji umbali wa kilomita 20 na shughuli zote za kujitafutia kipato
husimama.
“Maji ya
bwawa hilo sasa hivi huwezi kuona linatumiwa na jamii sababu ya mvua zinanyesha
madimbwi mengi yamejaa maji mvua ikiacha kunyesha vitongoji vyote sita hutegemea kwenye bwawa
la shule hiyo kwaajili ya kunywa na
matumizi mengine ambayo siyo safi na salama isitoshe jamii nayo imekuwa
ikijisaidia hovyo kwa kukosa vyoo ambavyo vimetitia kwa sababu ya mvua.
Mwenyekiti
wa kijiji hicho Buzali Mabele anasema kuwa
kweli kuna shida ya maji kwenye
kijiji hicho kilicho na vitongoji sita ambavyo ni mwamatembe,Mwasegagi,Mwakajala,Igunagahabi,Mwanjige
na Mwamajigi nakutegemea bwawa la shule walililichimba hivi sasa huwezi kuona
kama wanalihitaji sababu wanachota kwenye madimbwi mengine yaliyo na maji msimu
huu wa mvua.
“Lakini yakikauka
maji ya kwenye madimbwi
hulazimika kuchota maji ya bwawa
la shule pia ukosefu wa vyoo katika kaya
kujisaidia vichakani naona ni muda huu wa mvua kwani walikuwa na vyoo ingawa
vilikuwa havina ubora vimetitia sababu ya mvua kubwa kunyesha na ardhi ilivyo
ya kijijini hapo”anasema Mabele.
Mwalimu mkuu
wa shule hiyo Emanuel Magesa anasema
kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1981 na mpaka sasa ina jumla ya wanafunzi
480 wa darasa la awali pekee ni 90
na darasa la kwanza ni 112 ambao ni wengi na umri wao ni mdogo bado hawajafahamu matumizi ya
matundu ya vyoo hata katika mazingira wanayotokea ndani ya familia zao hilo
limekuwa changamoto hali iliyopo
wamekuwa wakijisaidia nje ya matundu ya vyoo
na katika mazingira ya shule ikiwa kuna bwawa la maji ambapo wamekuwa
wakielimishwa.
Mtendaji wa kijiji hicho Thomas
Nyonyo anasema kuwa bwawa la
shule lilichimbwa kwa nguvu za wananchi baada ya kupata mradi wa lishe shuleni
uliotolewa na shirika la lishe mwaka 2015 ambapo wanafunzi walihitajika
kupata chakula kilichokuwa kikipikwa shuleni hapo na kuwepo uhaba mkubwa wa
maji.
Nyonyo
anasema bwawa hilo limeweza
kuwasaidia wanafunzi kupata maji ya
kunywa na jamii ingawa kwa muda mfupi
kwani wanalazimika kuyafuata maji umbali
wa kilomita 20 halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kata ya Iselamagazi kijiji cha Ng’wang’osha.
Pia anasema
wakitaka kufuata maji katika kijiji cha Bunambiyu kuliko na bomba la maji safi
na salama ni umbali wa kilomita 15 kuyapata hivyo kwa wastani kijiji chote hakina maji zaidi
yakutegemea bwawa lililopo shuleni
ambapo maji yake nayo yanaonekana siyo safi na salama kutokana na mazingira
yake.
“Bwawa hilo
lililopo shuleni linahitaji utunzwaji na usimamizi mzuri ili kuepuka mlipuko wa
magonjwa katika jamii kwani hata upande
wa jamii yenyewe umekuwa hauna vyoo bora
hivi sasa kipindi cha mvua karibu
vyoo vingi kwenye kaya vimetitia
nakufanya kujisaidia vichakani hovyo kikiwepo cha shule chenye matundu mawili
nacho kimetitia pia”anasema mtendaji wa
kijiji Nyonyo.
Anasema
mpango uliopo ili kuweza kupata maji safi na salama ya kunywa
waliitisha kikao cha kijiji nakufikia maazimio ya kila kaya kuchangia
kiasi cha shilingi 50,000 ili kuyavuta bomba la
maji kutoka kijiji cha Bunambiyu
nakuweza kupata maji safi na salama
na wananchi wamedai wako tayari wakati watakapo uza mazao yao ikiwa
kijiji hicho kina kaya 218 na idadi ya
watu 1882.
Diwani wa
kata ya Bunambiyu Richard Sangisangi anasema kuwa kijiji hicho kweli hakina bomba kina shida ya
maji nani umbali mrefu kuyafuata maji
kwani hata haya yaliyopo hayatoshelezi kwa idadi ya watu waliopo kwenye kata nzima hata miundombinu ya bomba hilo sio imara limekuwa likihalibika mara kwa mara.
Mganga
msaidizi wa kituo cha afya Bunambiyu Simba Rajabu anasema kuwa idadi kubwa ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa kituoni
hapo huja na magonjwa ya kuhara idadi
kubwa ni watoto sababu ni kutokana na
mazingira wanayoishi nakutumia maji yasiyo
safi na salama .
Dkt Rajabu
anasema kuwa mara kwa mara wamekuwa wakiwapatia elimu juu ya afya zao na
mazingira wanayoishi ya ukosefu wa matundu ya vyoo au kuwa na vyoo bora kwani upande wa huduma za maji ni shida kwao hupata maji
yasiyo safi na salama katika vyanzo vya
maji na hawana desturi ya kuyachemsha ili kuua wadudu matokeo yake kupatwa na magonjwa ya mlipuko kama kuhara
walio wengi.
Mkurugenzi
wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Stephen Magoiga anasema kuwa kijiji hicho siyo pekee kuwa na
changamoto ya kukosa maji ni vijiji
vingi hilo linaeleweka ila mpango uliopo mradi wa
maji ya ziwa Victoria umeanza kuenea maeneo mengi jitihada zitafanyika
kuvuta mabomba ili kuwarahisishia wananchi huduma yakupata maji karibu kwa
mujibu wa sera ya maji nakuondokana na
kutafuta maji umbali mrefu.
Anasema lipo suala la
jamii kukosa vyoo vyenye ubora na
msimu wa mvua kweli vimetitia na matokeo
yake baadhi yao kuendelea kujisaidia
vichakani bila ya kujenga wanaweza kueta
athari kwenye vyanzo vyao vya maji
lakini bado wanaendelea kila siku kuwapatia elimu juu ya utunzaji
mazingira nakujenga vyoo vyenye ubora ili
kuepuka mlipuko wa magonjwa kama kipindupindu na kuhara.
Halmashauri
ya wilaya ya Kishapu ni miongoni mwa maeneo hapa nchini ni kame
yasiyopata mvua za kutosha ambapo
asilimia 88 ya wakazi wake ni wafugaji na wakulima na asilimia 27 ni wakulima pekee.
Hata hivyo Sera
ya maji ya mwaka 2002 inaeleza kuwa
uvunaji wa maji ya mvua ni njia muhimu yakupata maji hususani katika maeneo kame ambako
yanaweza kuwa ndio chanzo pekee cha maji
cha kuaminika katika kipindi cha
msimu wa kiangazi.
Pia moja ya
uvunaji ya maji wananchi wanaoishi vijijini watahamasishwa kutumia teknolojia hii ikiwa ukosefu wa maji safi na salama na kutofuata
kanuni bora za afya na usafi wa
mazingira ni chanzo kikubwa cha mlipuko wa magonjwa na vifo
na husababisha wimbi la umasikini
hasa kwa wanawake na watoto.
Hata hivyo
sera hiyo inaeleza kuwa ili kuboresha
afya ya jamii mkazo utawekwa
kwenye mipango ya pamoja
inayojumuisha utoaji wa
huduma za maji,usafi wa mazingira na elimu ya afya .
No comments:
Post a Comment