Mtandao huu bado upo kwenye matengenezo, punde utapata matukio katika picha, habari, makala na taarifa mbali za kijamii...Endelea kutufuatilia

Monday, May 21, 2018

MWAMKO MDOGO WA ELIMU KWA WAZAZI UMEFANYA KUTOTHAMNI ELIMU KWA MTOTO.


Na  Kareny  Masasy, Kishapu

MWAMKO  mdogo wa elimu  kwa wazazi wa  kata   ya Bunambiyu halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  imebainika  kuwarudisha nyumba maendeleo ya watoto wao kielimu kwa kuthamini  kuwatumikisha kazi za shambani  na kuchunga mifugo.
Licha ya hali hiyo pia wamekuwa wakiwaeleza wanafunzi wa kike  wafanye vibaya katika mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi ili wasifaulu  na baadaye waolewe lengo la mzazi kupata utajiri wa ng’ombe.
Mwalimu  mkuu wa shule ya msingi Ng’wang’hili  iliyopo kijiji hicho  Emmanuel  Magesa anasema kuwa  kumekuwepo na mdodoko  wa wanafunzi kushindwa kumaliza shule  kwasababu yakupewa majukumu ya kuchunga mifugo.
Hata hivyo anasema kuwa  hali hiyo inasababishwa na  baadhi ya wazazi kuwa na mwamko mdogo wa elimu ambapo changamoto nyingine  wamekuwa wakihamisha watoto wao bila kutoa taarifa yoyote.
“Anasema mfano  waliopo darasa la saba sasa hivi walianza darasa la kwanza mwaka 2012  wakiwa 51 ambapo  wavulana ni  22 na wasichana ni 29  na  hadi leo hii  kuna wanafunzi 19 tu ambao wanatarajia kufanya mtihani wasichana 8 na wavulana 11”anasema  mwalimu mkuu wa shule hiyo..
Mwalimu Magesa anasema kuwa  mafanikio ya elimu bure  yamefanya uandikishaji  wa wanafunzi  wa darasa la kwanza kutoka wanafunzi  50 kwa miaka ya nyuma  hadi kufikia  wanafunzi 112 kwa sasa.
Pia  uandikishaji   wa darasa la awali  ulikuwa wanafunzi 25  zamani hadi  kufikia 100 ambapo idadi inaanza kupungua  taratibu pindi wanapoanza kuingia darasa la  tano hadi la saba sababu wameonekana kukua kwa kutumikishwa kazi za shambani na kuchunga mifugo.
Magesa anasema kumekuwepo na baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaeleza watoto wao wafanye vibaya siku ya mtihani  wakumaliza elimu ya msingi katika hali ya matokeo kuanzia mwaka 2015 shule hiyo  walimaliza wanafunzi  22 na wawili tu ndio waliofaulu kuendelea na elimu ya masomo ya sekondari.
Pia mwaka 2016  wanafunzi  waliofanya mtihani darasa la saba walikuwa 21 ambapo wavulana  ni tisa na wasichana 12 na wote walifaulu ikiwa mwaka 2017 waliofanya mtihani ni 19  na nane  hawakufaulu ambao wavulana ni watatu na wasichana ni watano.
Anasema  licha yakuwepo utoro wa rejareja unaosababishwa na miundombinu mibovu hasa kipindi cha masika ambapo darasa la awali na darasa la kwanza hawaji shule  na hata ukimrudisha mwanafunzi amfuate mzazi wake aje mzungumze ndio umempatia  unafuu wa mwanafunzi kuendelea kukaa nyumbani na mzazi haji.
Mwanafunzi wa shule ya  msingi Ng'wang'hili  kata ya Bunambiyu aliyeacha shule  akiwa darasa la tano  nakuendelea kuchunga mifugo ya wazazi wake.  Picha na Kareny  Masasy.

Baadhi ya wazazi wa kata ya Bunambiyu   Modesta Obedi na Ernest Hausa wanasema kuwa wazazi wamekuwa wakishikwa na tamaa ya kupata utajiri wa ng’ombe kwani wamekuwa wakiwaeleza wanafunzi wa kike kufanya vibaya katika mitihani yao ya mwisho ili waweze kuolewa na mzazi kumiliki ng’ombe jambo ambalo anaona ni ufahari kwake.
Ernest Hausa anasema kuwa  kweli wapo wazazi wanaowatumikisha wanafunzi kazi za shambani msimu wa kilimo anaona wanao uwezo wa kulima msimu wa mvua umefika hakuna nguvu kazi bora aende akamuombee ruhusa shuleni kwa kusema uongo  nakumtumikisha  kuliko apate elimu.
Licha ya suala la  uchungaji mifugo  pia anasema  huwatumikisha shambani kwaajili yakulima vibarua  kwenye shamba la mtu nakupata fedha za  chakula msimu wa mvua  za masika kipindi cha kilimo.
 Mwenyekiti wa kijiji  cha  Ngw’ang’hi  Buzali Mabele anasema kuwa  wazazi wamekuwa wakiwaachisha shule watoto wao ili kuchunga mifugo na kulima au kuhama bila kutoa taarifa na kuwaozesha umri mdogo  hilo sasa limeingizwa kwenye mpango mkakati wa kijiji kuzibiti hali hiyo  isiendelee kwa kuwachukulia hatua za kisheria.
Mtendaji wa kijiji  cha   hicho  Thomas  Nyonyo anasema kuwa hivi sasa wameanza kuzibiti utoro kwa  kuwasaka wazazi ambao wanahama kimya kimya  na watoto wao ambao wanasoma shule  na kuwaeleza kuacha tabia ya kuwarubuni wafanye vibaya kwenye mitihani yao yakumaliza elimu ya msingi.
Wengine wazazi wamekuwa wakiwatumikisha shughuli za  shambani na kuchunga mifugo kwa kuona kwenda shule ni kero kubwa kwani idadi kubwa ya wazazi hawajasoma isitoshe ni jamii ya wafugaji  hasa  wanaoishi katika kijiji  utakuta mwenye ng’ombe chache ni 50.
Diwani wa kata ya Bunambiyu  Richard Sangisangi anasema kuwa kweli wazazi bado wanamwamko mdogo wa elimu wamekuwa  wakiwaachisha watoto wao kwenda shule ili wafanye kazi za shambani au kuchunga mifugo hilo limepigwa marufuku atakaye  bainika  mzazi atachukuliwa hatua na miundomibu ya barabara  msimu wa mvua unachangia utoro wa rejareja kwa wanafunzi.
Mkuu  wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba anasema kuwa  suala la wazazi wafugaji kutoruhusu watoto wao kwenda shule  hilo lipo ila walikuwa wakielezwa umuhimu wa elimu na kuwachukulia hatua wazazi watakao bainika kufanya kitendo hicho.
Hata hivyo Talaba anasema kuwa tayari yamekwisha tolewa maagizo  kwa  watendaji wa vijiji na kata kufuatilia wanafunzi watakao  watoro wanaosababishwa na kutumikishwa kazi mashambani na kuchunga mifugo ili wazazi waweze kuchukuliwa hatua  za kisheria.
“Kweli jamii ya wafugaji watoto wao wamekuwa hawasomi na wilaya hii asilimia 88 ni wafugaji na wakulima  ndio wanategemea kwa kuwainulia kipato lakini tabia ya kutowaombea  uhamisho shuleni  ipo, hata ukitaka kuwachukulia hatua wazazi unashindwa  utawapatia wapi?”alisema  mkuu wa wilaya.
Mkurugenzi Mtendaji  halmashauri  ya Kishapu Stephen Magoiga anasema kuwa  baadhi ya wazazi wamekuwa wakienda shuleni kuwaombea ruhusa watoto wao wanaumwa kumbe ni uongo wamekuwa wakifanya hivyo lengo kuwapeleka shambani kulima au kulichunga mifugo.
“Kuna mzazi mmoja tulielezwa amemuombea ruhusa mwanaye kuwa anaumwa lakini tulifuatilia mpaka shambani alipoenda yeye na mwanaye tukamkuta shambani mzazi huyo alichukuliwa hatua lakini aliomba msamaha kuwa  hatorudia tena  tena  ambapo ndio imekuwa tabia ya  baadi yao wazazi”alisema mkurugenzi.
Hata hivyo mkurugenzi Magoiga anasema kuwa kuna shule  za msingi 117  ambazo baadhi yao  maeneo yalipo  wanafunzi kweli wanalazimika kutembea umbali mrefu  hasa kijiji ch Ng’wang’hili  vitongoji vyake viko mbalimbali kwani wanafunzi wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita  zaidi ya saba kwenda shule nalo linasababisha utoro au kuacha shule.
Anasema  halmashauri hiyo matokeo ya darasa la saba kwa mwaka jana walishika nafasi ya mwisho kimkoa  katika halmshauri sita zilizopo hivyo ni jitihada zinahitajika baada ya kuweka mkakati kwa mwaka huu  kwa mwalimu mkuu  ambaye shule yake ikifelisha idadi kubwa  ataondolewa kwenye nafasi hiyo.
 Katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania  ya mwaka 1977 inaeleza kuwa  mtoto anahaki  ya kulindwa na kupendwa ,anayo haki ya  kupata elimu,kucheza na kujieleza  pia serikali imekomesha utumikishwaji wa watoto mashambani wala katika biashara ndogondogo

No comments:

Post a Comment