Mtandao huu bado upo kwenye matengenezo, punde utapata matukio katika picha, habari, makala na taarifa mbali za kijamii...Endelea kutufuatilia

Wednesday, January 31, 2018

BISHAGAZI: KISA MAFUNZO CHA HARAKATI NGAZI YA JAMII

Utangulizi:
Selemani Bishagazi ana umri wa miaka 39, anaishi Mtaa wa Kipunguni, kata ya Kipunguni, wilaya ya Ilala, mkoa wa Dar es Salaam. Mwaka 2011 alianza kujishughulisha na harakati za haki za binadamu bila ya yeye mwenyewe kujua kama anachokifanya ni harakati hizo.

 Anajishughulisha na biashara ya kuuza nguo za kike za mitumba maeneo ya Ubungo External (Mabibo Hostel) kama sehemu ya kujipatia kipato cha kuendesha maisha yake ya kila siku. Bishagazi ana mke na watoto.
Msaada wa cherehani



“Sherehe za kuwapongeza watoto wa kike baada ya kufanyiwa ukeketaji zilikuwa zikifanyika hadharani kwenye maeneo ninayoishi ya Kipunguni, walikuwa wakieleza wazi kabisa dhumuni la sherehe hizi. Jambo hili nilipokuwa nikilishuhudia, ndipo nilipoanza kuona kwamba haliko sawa” anaeleza Bishagazi.
Nilianza kulishughulikia sula hili kwa kwenda kuwaona viongozi wa serikali ya mtaa, mheshimiwa diwani na hata polisi, lakini kote huko sikupata ushirikiano wowote. Kwa mfano Mh. Diwani aliwahi kunitamkia wazi kwamba yeye hataweza kulifuatilia jambo hili kwani wananchi wake watamnyima kura kwenye uchaguzi utakaofuata. Kwa upande wa jeshi la polisi ili uweze kuwatoa kituoni waende kwenye tukio ni lazima ulipe hela ya mafuta ya gari litakalowabeba kwenda huko; au umlipe posho askari utakayepewa kufuatana naye kwenda kwenye tukio. Haya yote yalikuwa ni changamoto kwangu. Lakini pia kulikuwa na maneno ya kukatishwa tamaa kutoka kwa watu mbali mbali na wengine wakidiriki hata kuniambia “anayekeketwa siyo mwanao wala nduguyo, kinakuuma nini?” Lakini yote haya hayakunikatisha tamaa.
Bishagazi alianza kushiriki semina za jiansia na maendeleo maarufu kama GDSS Mwezi Septemba mwaka 2013, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.Alifahamu semina hizo kupitia mteja wake katika biashara zake. Katika maongezi  ya kawaida nilimdokeza kuhusu tatizo la ukeketaji kwenye maeneo anayoishi  ya Kipunguni. Hapo alishauriwa kuhudhuria semina za kila jumatano (GDSS) zinazofanyika TGNP Mtandao.Mteja huyo akasisitiza kwamba akihudhuria semina hizi atapata uelewa zaidi, lakini pia huenda aikapata msaada wa namna ya kutatua tatizo la ukeketaji Kipunguni na namna ya kuendesha harakati zaidi.
Semina hizo zimesaidia sana kuinua kiwango chake cha uelewa wa masuala mbambali, kujitambua,kujia thamani yake  kama binadamu na raia wa Tanzania,haki na thamani ya wasichana na wanawake.kikubwa zaidi amegundua kwamba harakati zozote zile kuleta mabadiliko huwezi kuzifanya peke yako, lazima ujenge nguvu za pamoja.
Akiwa kama kiongozi wa kikundi cha sauti ya  wananchi Kipunguni,wameweza kuokoa wasichana kadhaa lakini mmojawapo ni msichana Anna Nicolaus wa Kipunguni Gongo la Mboto jijini alishawishiwa na wazazi wake ili akubali kukeketwa kwa madai ya kuwa watampatia cherehani.Yeye alikimbia nyumabani na kukimbialia kwa Bishagazi ambaye alimpokea  na kushirikisha wanaharakati wengine ili waone ni kwa jinsia gani watamsaidia.Waliamua kwenda kwa mzazi ambaye ni mama na kumwelimisha madhara ya ukeketaji ndipo akatengua maamuzi yake ya kumkeketa binti yake.
Baada ya kipindi cha miaka miwili kikundi cha sauti ya wananchi kipunguni kilipata ugeni kutoka TGNP Mtandao,kati ya mamabo waliyovutiwa nayo ni kisa cha bi Anna na wakaahidi kuchanga fedha lili kumpataia Anna Charahani.Hatimaye ndoto ya Anna ikatimia kwani tarehe 15 mwezi wa sita aliweza kukabidhiwa na diwani wa kata hiyo Mh Mohamed Msophe charahani yake ambayo itampa ajira  kuendesha maisha yake na kujikwamua kiuchumi.Kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo akikwemo diwani wa kata ya Kipunguni

Mafanikio ndani ya Jamii ya Kipunguni:
·      Mradi wa Maji Kata ya Kipunguni
 Sauti ya Jamii Kipunguni ina wanachama zaidi ya 60 kutoka mitaa mine ya Kata ya Kipunguni;kwa kushirikiana na wanajamii wameweza kutatua  changamoto ya upatikanaji wa maji.Kutokana na uhaba wa maji  wanawake na watoto walitembea umbali mrefu ,watoto  kubakwa, kinamama kupata vipigo kutoka kwa waume zao na  mmoja wa wasichana aliyekwenda kuchota maji Mto Mzinga, na huko akachukuliwa kwa lazima na kwenda kukeketwa.
Mchakato ulianza kwa kukusanya taarifa hizo na nyingine zilizokuwepo na kuzipeleka kwa Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa ambaye alileta mradi mkubwa wa maji kwenye Kata ya Kipunguni wenye thamani wa Shs. 890m/=. Ushawishi huu ulifanyika mwaka 2014, na hivi sasa mradi uko kwenye hatua za mwisho kukamilika. Mradi huu utasambaza maji sehemu kubwa ndani ya Kata yetu ya Kipunguni.

·      Kilimo cha Mboga Mboga kwa Kinamama
Kwa ushawishi wa Bishagazi ameweza kuwaunganisha wanawake 24 (mmoja wao akiwa ngariba) wakaanzisha kilimo cha mboga mboga, na kilimo hiki kwa sasa kinawasaidia kupata mboga majumbani mwao, lakini pia wanauza mboga ya ziada na kujipatia kipato. Alianza kwa kuwakodisha eneo lenye ukubwa wa ekari 3 kwa Shs. 150,000/= ambalo sehemu ya eneo hili linatumika kwa kilimo hiki. Kwa sasawanawake hawa wanakodisha eneo hilo kwa gharama zao. Eneo hili liko bondeni na kuna chem chem ya maji inayotumika kumwagilia mboga. Lakini pia kutokana na ufugaji wa kuku katika maeneo ya jirani wanaweza kupata mbolea  kwa ajili ya kilimo chao cha mboga.

Sauti ya Jamii Kipunguni hukitumia kupenyeza agenda mbalimbali ikiwemo ya kupambana na ukeketaji. Wamekuwa wakizungumza nao ana kwa ana kuhusu ukeketaji na madhara yake, na umuhimu wa kuachana na mila hii potofu. Lakini pia wakipata machapisho mbalimbali kutoka TGNP na taasisi zinginezo.

·      Upotevu wa Ushuru wa Serikali Machinjio ya Mazizini
 Sauti ya Jamii Kipunguni ilipata taarifa kuhusu ufisadi unaofanyika kwenye machinjio ya Mazizini yaliyoko kata ya Kipunguni. Ushuru unaolipwa kwa ajili ya kuchinja ng’ombe machinjioni hapo kiasi kikubwa kinaishia kwenye mifuko ya wajanja wachache ambao ni viongozi wa machinjio hayo, badala ya kwenda serikali kama inavyotakiwa. Kwa mfano kila ng’ombe anayechinjwa Mazizini hulipiwa Shs. 10,000/=; lakini hakuna risiti yoyote ya serikali inayotolewa kwa mlipaji Mh. Mwigulu Nchemba alifanya ziara ya kushtukiza kwenye machinjio ya Vingunguti na kujionea mwenyewe ufisadi mkubwa uliokuwa ukifanyika hapo. Waziri Mwigulu alitoa maelekezo kwamba mara moja machinjio zote zitumie mashine za kielektroniki (EFD) kutoza ushuru wa machinjio ili kuepusha upotevu wa mapato machinjioni. Suala hili halikuishia hapo kwani niliweza pia kulipeleka na kulizungumzia kwenye vyombo vya habari kama ITV, Radio One, East Africa Radio na gazeti la Nipashe.

·      Kujengea Uwezo Wananchi na Kuwajibisha Viongozi:

Kwa wastani sauti ya jamii Kipunguni imeweza  kuwafikia watu 1,500 na  kuwajengea uwezo wa masuala mbali mbali na kwa kiwango tofauti tofauti ndani nan je ya Kata ya Kipunguni. Hawa ni pamoja na wananchi wa kawaida, viongozi wa kisiasa, viongozi wa serikali, watumishi wa umma (walimu, polisi), viongozi wa vikundi na taasisi za kijamii, wazee, wanawake, watoto wa kike, wapiga kura n.k.Pia wameweza kuwasainisha mikataba ya makubaliano ya madai ya wanachi/wapiga kura na baadhi ya wagombea wa nafasi za uongozi ili pindi watakapopata nafasi hizi za uongoi watekeleze yale waliyokuabaliana  na kutia sahihi zao kabla wanachi hawajawapigia kura.

No comments:

Post a Comment